KONGAMANO LA KITAIFA LA NGURUWE KUFANYIKA TANZANIA
KONGAMANO LA KITAIFA LA NGURUWE KUFANYIKA TANZANIA
Na. Chiku Makwai (MUV). Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikishirikiana na chama cha wafugaji wa Nguruwe Tanzania (TAPIFA) imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa kongamano la kimataifa la ufugaji wa nguruwe litakalo fanyika Septemba 11-13, 2025 jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa leo Aprili 16, 2025 na Naibu Waziri, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari Uliofanyika katika Ukumbi uliopo jengo la NBC jijini Dodoma.















